KOCHA MKONGOMANI WA YANGA ANYANG'ANYWA JEZI YENYE LANGI YA SIMBA AAMBIWA HIVI

Baada ya kuwasili jana mjini Morogoro na kupata nafasi ya kukinoa kikosi cha Yanga kwenye Uwanja wa Chuo cha Biblia, jezi ya Kocha Mkongomani Mwinyi Zahera yawa gumzo kwa baadhi ya mashabiki wa timu zote mbili.

Zahera alitinga Uwanjani kuishuhudia timu yake mpya akiwa amevalia uzi mweusi wenye micharazo ya rangi nyekundu kwenye mabega, rangi ambayo haijawahi kutumika kabisa katika klabu hiyo yenye maskani yake katika mitaa ya Twiga, iliyo Jangwani, Kariakoo.

Baadhi ya mashabiki ikiwemo wale wa Yanga na Simba, wamekuwa wakihoji imekuwa avae rangi ambazo hazitumiki ndani ya klabu.

Wapo wale walioandika mitandaoni haswa wa upande wa pili wakitupa vijembe kuwa Mkongo huyo ana damu ya Simba kutokana na rangi hiyo nyekundu.

Rangi ya Yanga ambayo inatambulika siku zote ni kijani na njano, pia hivi karibuni wamekuwa wakitumia nyeusi haswa katika mechi za ugenini.

Kitendo cha Zahera kuvaa rangi hiyo ambayo hutumiwa na watani zao wa jadi Simba, imekuwa gumzo kubwa zaidi kwa baadhi ya mashabiki ambao hawajawahi kuiona ikitumika Jangwani.

Comments

Popular posts from this blog

YANGA YASAFIRI NA HAWA TU , WENGINE WOTE WABAKI NCHINI

YANGA YAJIBIWA HIVI NA TFF KUHUSU KUOMBA KUJITOA KAGAME CUP

MASHINDANO MENGINE TOFAUTI NA KAGAME KUANZA 29, JUNE SIMBA NA YANGA NDANI RATIBA NZIMA HII HAPA