Posts

kiwalinews

HISTORIA YA KABILA LA WAFIPA KUTOKA SUMBAWANGA

Image
WAFAHAMU WAFIPA.. Wafipa ni jamii ya wabantu waishio katika mkoa wa Rukwa. Shughuli kuu za uchumi kwa jamii hii ni kilimo na ufugaji. Baadhi hujishughulisha na uvuvi na uwindaji.na wale wanaoishi pembeni mwa mto Rukwa hujishughulisha na uvuvi kama moja ya shughuli za kiuchumi. Wafipa wana historia ndefu hasa katika teknolojia ya ufuaji wa chuma kuanzia arne ya 17. Kama ilivyo kwa jamii nyingi, mila na desturi za wafipa ni suala linaloheshimiwa. Ndoa hufanywa kwa kufuata taratibu za kimila. Kijana akifikia umri wa kuoa hushauriwa na wazazi wake kuhusu ukoo mzuri wa kutafuta mke. Masuala yanayozingatiwa ni pamoja na kuchapa kazi, kuepuka koo zenye magonjwa na zisizokuwa na uzao. Kijana akishaoa hukaa karibu na wazazi kwa muda wa mwaka mmoja ili kujifunza jinsi ya kuendesha familia baada ya hapo huweza kujenga sehemu nyingine. Wafipa: Kabila lililoamini uwepo wa Mungu wa mbinguni... WAFIPA ndilo kabila kubwa kuliko mengine yaliyopo katika mkoa wa Rukwa. Makabila mengine ni

MABINGWA WA Dr. SHOO CUP EDU 3 WALIVYO PEWA HESHIMA YAO KAMA MABINGWA

Image
Bofya hapa kutazama video Mabingwa wa Dr. Shoo Cup Chuo kikuu cha Makumira ambao Ni team ya Education Mwaka wa tatu leo wamepewa heshima yao Kama mabingwa (Guard of honor ) na team ya kitivo cha Sheria Mabingwa hao wamepewa heshima hiyo pale walipo kutana kwenye mechi ya Kirafiki ambapo mtanange huo ulimalizika kwa Mabingwa hao kuibamiza team ya kitivo cha sheria kwa mabao 4 - 1.  Huku magoli hayo ya mabingawa yakiwekwa kambani na Kenny ambaye alitupia magoli 2 katika kipindi cha kwanza huku magoli mengine mawili yakifungwa katika kipindi cha pili na washabuliaji Samba ambaye alifunga goli amaizing sana goli lililomfanya hadi kocha wa team pinzani akashangilia uwezo na umalidadi wa mfungaji  huku goli la nne likiwekwa kambani na Cheche Mnamo dakika za majeruhi team ya sheria waliweza kupata goli moja la kufutia machozi kupitia kwa kiungo wao Medy ambaye alifunga goli baada ya kipa wa mabingwa kutema mpira uliopigwa Kama faul Kuitazama video hii bofya hapo chini BOFYA HAPA KU

INGIA SARIS KUPITIA LINK HII

Image

TSHISHIMBI KUTOKA YANGA KWENDA SIMBA AZUNGUMZA HAYA

Image
Kiungo Papy Tshishimbi ameondoka nchini na kurejea kwao DR Congo kwa ajili ya mapumziko. Tshishimbi amekuwa akihusishwa na kujiunga na Simba, jambo ambalo limewapa hofu na hasira baadhi ya mashabiki wa Yanga. Tshishimbi hakuwa amewahi kulizungumzia suala hilo lakini jana amekutana na Salejembe jijini Nairobi, Kenya na kuweka wazi kila kitu. Tshishimbi amesema anareja kwao kwa mapumziko akiwa bado ni mchezaji wa Yanga na atarejea baada ya mapumziko. Kuhusiana na suala la Simba, hii ndiyo kauli yake. “Kuhusu Simba ninasikia tu kwa kweli. Lakini hakuna ambaye amewahi kunifuata tukalizungumzia suala hilo.” Alipoulizwa kama Simba wakimfuata, yuko tayari kujiunga nao? “Soka ni biashara rafiki yangu, unajituma na kufanya vizuri ili upae kibiashara na kujiendeleza zaidi. Timu ikifanikiwa, soko linakuwa juu. “Kama Simba wananihitaji, niko tayari wanaweza kusema wanahitaji nini nami niangalie.”

SIMBA KUWEKA KAMBI ITALY ENDAPO

Image
Imeelezwa kuwa kikosi cha Simba kitasafiri kuweka kambi nchini Italia endapo kitafanikiwa kutwaa ubingwa wa Sportpesa Super Cup nchini Kenya. Taarifa kutoka ndani kutoka klabu hiyo zimeeleza mabingwa hao wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2017/18 wataelekea nchini Italia kwa ajili ya kambi ya maandalizi ya msimu ujao wa ligi. Kikosi hicho kesho Jumapili kitakuwa kinashuka Uwanja wa Afraha mjini Nakuru, Kenya kucheza fainali ya SportPesa Super Cup dhidi ya Gor Mahia FC. Simba walitinga hatua huyo baada ya kuwaondosha Kakamega HomeBoyz kutoka Kenya na Gor Mahia wakiiondoa Singida United ya Tanzania. Fainali ya mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu na wadau wengi wa soka la Tanzania na Kenya utaanza majira ya saa 9:00 alasiri

HUYU NDO KOCHA MPYA WA SIMBA ANAE MRITHI PIEERE LECHANTRE

Image
Inaelezwa kuwa mabosi wa klabu ya Simba wameanza mazungumzo na Mfaransa mwingine atakayerithi kiti cha Pierre Lechantre ambaye amenyimwa mkataba wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo. Taarifa za ndani zinasema Hubert Velud ni jina la kocha ambaye anahusishwa kuja kuinoa timu hiyo yenye maskani yake maeneo ya Kariakoo jijini Dar es Salaam. Velud amewahi kuzinoa klabu kubwa barani Afrika ikiwemo Etoile du Sahel, ES Setif, TP Mazembe pia timu ya taifa ya Togo. Mfaransa huyo anaweza kuja nchini kuchukua nafasi ya Mfaransa mwenzake ambaye mkataba wake umeshamalizika baada ya kusaini miezi 6 inayomalizika siku chache zilizosalia. Na taarifa zilizopo kwa wekendu hao wa Msimbazi ni kuwa tayari wameshaachana na Lechantre kutokana na kutorodhishwa na kiwango chake ndani ya timu na sasa wameanza mazungumzo na makocha wengine ikiwemo Velud anayehusishwa. 09 Jun 2018

SIMBA WAACHANA NA LECHANTRE KIIVI

Image
Na Mwandishi Wetu,   NAKURU KOCHA Mfaransa wa Simba SC, Pierre Lechantre na Msaidizi wake, Mtunisia Aymen Hbibi Mohammed wameondoka kwenye kambi ya timu nchini kurejea Dar es Salaam kuunganisha usafiri wa kurudi kwao – maana yake kazi basi. Simba SC inaendeleza ugonjwa wake wa kutodumu na makocha baada ya kutofautiana na Lechantre aliyeanza kazi Januari 18 tu, mwaka huu. Lechantre na Aymen Hbibi Mohammed jana walikuwa jukwaani wakati Simba SC ikimenyana Simba SC na Kakamega Homeboyz katika Nusu Fainali ya SportPesa Super Cup na kuibuka na ushindi wa penalti 5-4 baada ya sare ya 0-0 ndani ya dakika 90 Uwanja wa Afraha pia. Timu iliongozwa na Kocha Msaidizi, Mrundi Masoud Juma aliyekaa benchi na kocha wa makipa, Muharami Mohammed ‘Shilton’ na jukwaani alikuwepo Kaimu Rais wa klabu, Salim Abdallah ‘Try Again’. Dalili za Simba SC kutodumu na kocha huyo zilianza kuonekana mapema tu baada ya Lechantre kuomba kazi ya kuifundisha timu ya taifa ya Cameroon Aprili mwaka huu. Na b