ZAWADI NONO HII HAPA KWA WACHEZAJI WA SIMBA ENDAPO WATATWAA UBINGWA SPORT PESA



Hatimaye klabu ya Simba imefunguka na kusema fedha zote za ubingwa wa Sports Pesa Super Cup watapewa wachezaji.

Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema fedha zote dola 30,000 (zaidi ya Sh milioni 66) kama watabeba ubingwa zitakuwa mali ya wachezaji.

“Tayari tumezungumza nao na kuwaeleza kuhisiana na suala hilo kwamba fedha zote zitaenda kwao,” alisema.

Manara amesema hayo mara tu baada ya Simba kushinda kwa mikwaju ya penalti na kutinga nusu fainali.

Simba imeing’oa Kariobang Sharks kwa penalti 3-2 baada ya mechi kwisha bila bao katika dakika 90.

Comments

Popular posts from this blog

YANGA YASAFIRI NA HAWA TU , WENGINE WOTE WABAKI NCHINI

YANGA YAJIBIWA HIVI NA TFF KUHUSU KUOMBA KUJITOA KAGAME CUP

MASHINDANO MENGINE TOFAUTI NA KAGAME KUANZA 29, JUNE SIMBA NA YANGA NDANI RATIBA NZIMA HII HAPA